Kurasa

Jumapili, 18 Februari 2018

RASIMU YA KATIBA YA MARAFIKI WA ELIMU KANDA YA ZIWA


RASIMU YA KATIBA YA MTANDAO WA

MARAFIKI WA ELIMU KANDA YA ZIWA (FENLZ),

TOLEO LA KWANZA 2017.

SEHEMU YA KWANZA:

IBARA YA 1: UTANGULIZI:

Sisi Marafiki wa Elimu wa Kanda ya ziwa ambao ni muunganiko wa Marafiki wa Elimu waishio katika kanda ya ziwa kwa hiari yetu tumeamua kujiunga kisheria ili kushughulikia masuala ya kuboresha Elimu, Demokrasia, Utawala bora na mawasiliano katika jamii ya Kanda ya ziwa kwa kushirikiana na wananchi wa kada zote na wadau mbalimbali.

Asasi hii imeanzishwa kwa matakwa ya Marafiki wenyewe kwa lengo la kujihusisha na kuelimisha jamii ili kuboresha elimu na demokrasia bila shinikizo toka kwa wanasiasa, vikundi vya dini au ukabila. Asasi hii itatekeleza majukumu yake kwa kuzingatia sheria za nchi kanuni na taratibu za mashirika yasiyo ya kiserikali nchini Tanzania.

IBARA YA 2: JINA LA KATIBA NA ANUANI NA UTUMIKAJI:

2.1.Jina la Katiba.

Katiba hii ni waraka halali wa FENLZ, hivyo itajulikana na kutambulika kwa jina la katiba ya “Marafiki wa Elimu Kanda ya Ziwa”

           

2.2. Anuani ya FENLZ itakuwa:-

         Mtandao wa Marafiki wa Elimu Kanda ya Ziwa,

            S. L. P                 Mwanza

 

2.3.Tarehe rasmi ambayo katiba hii itaanza kutumika.

Katiba hii itaanza kutumika mara baada ya kupata usajli rasmi na wanachama wa FENLZ na kufanya uchaguzi wa viongozi kwa mujibu wa katiba hii.

 

3.      LUGHA YA ASASI:

Kwa kuwa FENLZ ni asasi huru yenye wanachama wenye viwango tofauti vya elimu; na kwakuwa FENLZ inafanya kazi na watu wa kada tofauti: lugha kuu ya mawasiliano itakuwa Kiswahili na lugha ya pili itakuwa Kiingereza

 

SEHEMU YA PILI:

 

DIRA, DHAMIRA, MADHUMUNI NA ULINZI WA ASASI:

4.      Dira ya FENLZ:

Nikuwa na Kanda ya ziwa yenye mazingira bora ya elimu, utawala bora, Demokrasia ya kweli kwa wananchi wote mfumo bora na imara wa mawasiliano ndani ya jamii.

 

5.      Dhamira ya FENLZ

Kuwezesha upatikanaji wa taarifa sahihi kuhusiana na changamoto za elimu, Demokrasia na Utawala bora na namna ya kushirikiana na serikali na jamii kuzikabili changamoto hizo ili kuleta mafanikio chanya kwa manufaa ya umma.

 

6.      Madhumuni ya FENLZ.

6.1.      Kufanya ufatiliaji na uchambuzi wa masuala ya elimu, demokrasia, utawala bora na kuimarisha mfumo wa mawasiliano katika jamii na vyombo vya utawala.

6.2.      Kutoa elimu kwa jamii juu ya umuhimu wa ushiriki wao katika mikutano kwa manufaa ya kijamii na kukabiliana na changamoto za maendeleo katika maeneo yao.

6.3.      Kuendesha midahalo, mikutano, mijadala, na makongamano ya kijamii juu ya masuala mbalimbali na kukabiliana na changamoto za maendeleo.

6.4.      Kutumia vyombo vya habari kama redio, TV na magazeti kuelimisha jamii.

6.5.      Kujihusisha kikamilifu katika kusaidia jamii kitaaluma na ushauri katika masuala yanayo kwamisha maendeleo yao.

6.6.      Kutoa elimu kwa jamii hususani vijana wa shule za Msingi, Sekondari na vyuo pamoja na walio nje ya shule kuhusiana na haki zao za msingi, elimu ya afya ya uzazi, elimu kuhusiana na VVU/UKIMWI, magonjwa ya ngono, madhara ya matumizi ya dawa za kulevya na sigara, elimu ya ujasiriamali na kuinua kipato, pamoja na masuala  mtambuka kama mazingira

6.7.      Kutoa elimu ya Demokrasia, Utawala bora na Usawa wa kijinsia katika jamii.

6.8.      Kuanzisha klab za Marafiki wa Elimu ndani na nje ya shule za Msingi, Sekondari na Vyuo kwa ajili ya kujadili masuala mbalimbali ya elimu, demokrasia na utawala bora katika jamii.

 

7.      ULINZI WA ASASI:

Asasi hii itatekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria zilizowekwa na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; na dhamira  yake ya kutekeleza shughuli zake kwa mujibu wa katiba yake na sheria za Tanzania.

 

SEHEMU YA TATU

KATIBA, USAJILI NA ENEO LA UTENDAJI KAZI:

 

8.      Katiba

            Katiba ya FENLZ ndio muongozo wa shughuli zote za Asasi hii.

 

9.      Jina la Asasi         

            Asasi hii itaitwa MTANDAO WA MARAFIKI WA ELIMU KANDA YA ZIWA kwa kifupisho FENLZ.

 

 

10.  Usajili

Baada ya kusajiliwa; makao makuu ya FENLZ yatakuwa katika mji wa Mjini Mwanza katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

 

 

11.  Eneo la utendaji kazi

            FENLZ itafanya kazi katika maeneo ya Kanda ya Ziwa, kwa kuhusisha ngazi mbalimbali za uanachama na marafiki wa mtandao huu

 

12.  Washirika wa FENLZ.

            FENLZ itakuwa na haki ya kushirikiana na Taasisi, Mashirika mbalimbali ndani na nje ya Tanzania, watu binafsi, makampuni na Asasi nyingine ambazo zitakuwa na nia ya  kusaidia na kushirikiana na FENLZ katika kutekeleza Dira na Dhamira ya FENLZ.

 

13.  Kanuni za Kimaadili.

13.1.  Katika kutekeleza majukumu yake; FENLZ itazingatia maadili, uadilifu, nidhamu, uwajibikaji kujituma, kujitolea na uchapakazi kwa manufaa ya taifa.

13.2.  Wanachama na viongozi wa FENLZ lazima wawe waadilifu.

 

 

SEHEMU YA 4:

AINA ZA UANACHAMA WA FENLZ:

 

14.  UANACHAMA.

            Kutakuwa na aina tatu tu za uanachama wa FENLZ kwa mujibu wa katiba hii ambazo ni;

 

14.1Wanachama  waanzilishi

Huu ni uanachama wa watu walishiriki katika kuanzisha wazo la kuundwa kwa FENLZ na ambao kwa namna moja au nyingine walifanikisha FENLZ kupata usajili.

 

14.2Wanachama binafsi

14.2.1    Huu ni uanachama wa mtu binafsi ambaye kwa mapenzi yake atapendezwa na shughuli za FENLZ na kuamua kujiunga kuwa mwanachama kwa hiari yake mwenyewe.

14.2.2    Kwa mujibu wa katiba hii, kuwa mwanachama wa FENLZ hakuunyimi kuwa mwanachama Wilaya, Mkoa wala Taifa.

 

14.3Uanachama wa Heshima

14.3.1    Mtu binafsi, shirika, kampuni au Taasisi yoyote wanaweza kuwa wanachama wa FENLZ kwa kuchaguliwa /kuteuliwa na kamati kuu ya uongozi ya FENLZ kisha kuandikiwa barua ya nia hiyo na iwapo watakubali watakuwa wanachama rasmi wa FENLZ.

14.3.2    Mwanacham wa heshima wa FENLZ hatapiga kura ya maamuzi juu ya jambo lolote linalohusu FENLZ.

 

15.  SIFA ZA MWANACHAMA:

15.1              Wanachama waanzilishi watatambuliwa kwa sifa zifuatazo:

15.1.1                                Awe ni mtu aliyejitolea kwa hali na mali katika kuanzishwa kwa FENLZ

15.1.2    Awe na nia ya dhati ya kuhakikisha kuwa atakuwa mstari wa mbele kutimiza Dira na Dhamira ya FENLZ.

15.1.3                                Atambue kuwa anapaswa kuitumikia FENLZ na si FENLZ imtumikie.

15.1.4                                Awe tayari kushirikiana na wadau wengine ili kulinda maslahi ya taifa

 

15.2              Mwanachama binafsi

15.2.1       Awe ni mtu mwenye kuziunga mkono kwa dhati shughuli na juhudi za FENLZ

15.2.2       Awe mwenye kujitoa kuitetea FENLZ ili kufanikisha malengo yake.

15.2.3       Awe na uwezo wa kuisaidia FENLZ kwa hali na mali pasipo kuchoka.

15.2.4       Awe mtu yeyote mwenye akili timamu na umri usiopungua miaka kumi na nane (18)

 

16.  HAKI ZA MWANACHAMA

            Wanachama wa FENLZ wana haki zifuatazo.

           

16.1          Kuhudhuria vikao vinavyo wahusu kwa mujibu wa katiba hii.

16.2          Kupata taarifa ya FENLZ kwa kufuata taratibu zilizopo.

16.3          Kushiriki katika vikao mbalimbali vya maamuzi ya FENLZ kwa mujibu wa taratibu.

16.4          Kuchaguliwa au kuchagua viongozi wa FENLZ kwa mujibu wa wa taratibu za Katiba.

16.5          Haki ya kujitetea na kujieleza kwa tuhuma/kosa alilotenda mbele ya vyombo vya FENLZ.

16.6          Haki ya kuteuliwa kuiwakilisha FENLZ katika maeneo/ shughuli mbalimbali.

16.7          Haki ya kupata taarifa na kuzitumia kwa manufaa ya FENLZ na jamii.

16.8          Haki ya kushiriki na kushirikisha uongozi na wanachama wa FENLZ katika mambo yenye manufaa kwa FENLZ na jamii.

16.9          Haki ya kuwa na nakala ya katiba ya FENLZ

 

 

17.  WAJIBU WA MWANACHAMA:

Wajibu wa mwanachama wa FENLZ ni pamoja na:,

17.1              Kulipa ada na michango yote ya FENLZ kwa ajili ya uendelevu wa Asasi.

17.2              Kuhudhuria vikao na mikutano yote inayohusu kwa mujibu wa katiba hii.

17.3              Kuwa mwaminifu, mwadilifu mkweli na kutetea msimamo wa FENLZ katika Maendeleo.

17.4              Kuchangia mawazo kwa hali na mali katika kulinda Dira na Dhamira ya FENLZ.

17.5              Kufahamu kwa undani katiba ya FENLZ

 

18: KUKOMA UANACHAMA:

                        Uanachama utakoma kwa:

18.1              Mtandao wa Marafiki wa Elimu Kanda ya Ziwa kufutwa kwa mujibu wa sheria za nchi.

18.2              Mwanachama kuamua kujiudhulu kwa hiari yake.

18.3              Kufukuzwa uanachama.

18.4              Kushindwa kulipa ada kwa kipindi cha mwaka mmoja bila sababu za msingi.

18.5              Kukiuka maadili ya uanachama wa FENLZ kwa makusudi.

18.6          Kwa kutenda kosa lolote ambalo wanachama wataridhia kwamba linafaa kumuondoa katika uanachama wa FENLZ na uamuzi huo kuridhiwa na mkutano mkuu.

 

SEHEMU YA TANO

MUUNDO NA WAJIBU WA VIONGOZI:

 

19:    MUUNDO NA WAJIBU WA VIONGOZI:

            Uongozi wa FENLZ utakuwa kama ifuatavyo

 

19.1              Mratibu wa FENLZ

19.2              Mwenyekiti wa FENLZ.

19.3              Makamu mwenyekiti wa FENLZ.

19.4              Katibu wa FENLZ.

19.5              Mweka hazina wa FENLZ

 

19.1 Mwenyekiti

            Wajibu wa mwenyekiti utakuwa kama ifuatavyo:

 

19.1.1    Mwenyekiti ataongoza Mikutano ya Bodi ya ushauri na mkutano mkuu wa Wanachama.

19.1.2    Mwenyekiti atakuwa msemaji mkuu wa FENLZ katika mikutano ya bodi ya ushauri na mkutano mkuu wa wanachama.

19.1.3    Aache hisia zake binafsi zikiangalia maamuzi ya wengi ila pale kunapokuwa na usawa wa maamuzi kwa pande mbili.

 

19.2          Makamu Mwenyekiti

19.2.1    Makamu mwenyekiti atafanya kazi za mwenyekiti kama mwenyekiti hayupo.

19.2.2                  Atafanya kazi za mwenyekiti kwa kuagizwa na mwenyekiti

19.2.3                  Kufuatilia utekelezaji wa maamuzi ya mikutano ya bodi ya ushauri na mkutano mkuu wa FENLZ.

 

 

19.3      Katibu

            Katibu atakuwa na kazi zifuatazo;

19.3.1                  Atatunza kumbukumbu za vikao vya bodi ya ushauri na mikutano ya FENLZ.

19.3.2                  Ndiye katibu wa mikutano ya kamati ya Bodi ya Ushauri na mkutano mkuu wa FENLZ.

19.3.3                  Katibu atawasiliana na mwenyekiti na makamu mwenyekiti kwa maamuzi ya utekelezaji.

19.3.4                  Kuandika barua na kuitisha vikao baada ya kuwasiliana na mwenyekiti.

19.3.5                  Kuandaa agenda za mikutano ya Bodi ya Ushauri, Mkutano mkuu na mikutano ya Dharula.

19.3.6                  Kuandaa taarifa mbalimbali za FENLZ na kuzipeleka pale zinapo hitajika

19.3.7                  Kuratibu shughuli mbalimbali za kamati ndogo ndogo za FENLZ.

19.3.8                  Kuratibu shughuli zote za kila siku za FENLZ.

 

19.4             Mweka Hazina

19.4.1                  Mweka hazina atakuwa na wajibu ufuatao;

19.4.2                  Atakuwa mtunzaji mkuu wa fedha za FENLZ.

19.4.3                  Atasimamia utunzaji wa vitabu vya kumbukumbu za fedha za FENLZ.

19.4.4    Kuaandaa na kutoa taarifa za fedha za FENLZ katika vikao vya Bodi ya Ushauri na Mkutano mkuu wa FENLZ.

19.4.5                  Atakuwa mdhamini wa mali za Asasi kwa niaba ya FENLZ

19.4.6                  Kushughulikia suala la utafutaji wa rasilimali fedha kwa ajili ya uendelevu wa FENLZ.

 

19.5      Mratibu wa FENLZ

 

19.5.1    Ndiye mratibu mkuu wa shughuli zote za FENLZ

19.5.2    Ndiye mkuu wa idara ya utafiti na mawasiliano ndani ya FENLZ

 

SEHEMU YA 6

UCHAGUZI NA MUDA WA KUKAA MADARAKAN.

20.              Muda wa Uongozi

Viongozi watakao chaguliwa kwa mujibu wa katiba hii watadumu madarakani kwa muda wa miaka miwili (2), lakini wanaweza kuchaguliwa tena kwa kiindi kingine.

           

21.              SIFA ZA KIONGOZI:

21.1.            Awe mwanachama wa FENLZ

21.2.            Awe na uwezo wa uongozi na kupambanua mambo

21.3.            Awe mwenye sifa na uwezo wa uongozi

21.4.            Mwenye kujituma

21.5.            Anaye kubali kutoa na kupokea ushauri toka kwa watu wengine walio wanachama na wasio wanachama wa FENLZ na kuufanyia kazi.

21.6.            Awe tayari kujitolea kuliko kutegemea mapato/ malipo toka FENLZ.

 

22.  KUONDOKA KATIKA UONGOZI:

            Viongozi wanaweza kuondoka madarakani kwa njia zifuatazo;

22.1.            Kutokuchaguliwa tena na wanachama

22.2.            Kujiuzulu

22.3.            Kupigiwa kura ya kutokuwa na imani na wanachama

22.4.            Kufukuzwa kutokana na makosa ya kukiuka katiba hii

22.5.            Kuhukumiwa kifungo jela kwa makosa ya jinai n.k

22.6.            Kupata maradhi ambayo yataathiri kabisa uwezo wake wa kutekeleza majukumu yake ya kila siku.

22.7.            Kufariki dunia.

22.8.            Kuhama makazi ya kudumu nje ya maeneo ya kanda ya ziwa

 

 

SEHEMU YA SABA

MIKUTANO NA VIKAO VYA FENLZ:

 

23.  MIKUTANO/VIKAO VYA FENLZ NA MAJUKUMU YAKE.

 

                        FENLZ Itakuwa na Mikutano/vikao kama ifuatavyo;

23.1.            Mkutano Mkuu

23.1.1.     Kutakuwa na mkutano mkuu wa wanachama ambao utafanyika mara moja kila mwisho wa mwaka.

23.1.2.     Mkutano utahudhuliwa na watendaji wote wa FENLZ, wanachama hai (waliolipa Kiingilio na ada), wanachama waanzilishi wa FENLZ, wanachama wa heshima na wageni mbalimbali watakao alikwa kuhudhuria.

23.1.3.     Mkutano mkuu ndio chombo chenye madaraka yote ya kuamua mambo muhimu ya FENLZ ikiwa ni pamoja na kupitisha sera na taratibu mbalimbali za kusimamia uendeshaji wote wa Asasi.

23.1.4.     Kuchagua mwenyekiti, makamu mwenyekiti, mweka hazina, na wajumbe wa bodi ya ushauri ya FENLZ pamoja na wajumbe wa kamati mbalimbali.

23.1.5.     Kupokea na kupitisha makisio ya mapato na matumizi ya FENLZ kutoka kwa mweka hazina.

23.1.6.     Kupitisha jina la mkaguzi wa mahesabu ya FENLZ.

23.1.7.     Kujadili na kupitisha taarifa za mwaka za utekelezaji wa shughuli za FENLZ.

23.1.8.     Kujadili na kupitisha mabadiliko ya katiba ya FENLZ.

23.1.9.     Kujadili na kupitisha mikakati na mipango ya muda mfupi na mrefu ya FENLZ.

23.1.10. Kufanya maamuzi yote ya FENLZ, kama itakavyo onekana inafaa.

 

23.2.                               Mkutano Mkuu wa dharura

23.2.1.  Mkutano wa dharura unaweza kuitishwa endapo kutakuwa na ombi lililotolewa na kutiwa saini na si chini ya theluthi mbili (2/3) idadi ya wanachama na kuweka bayana katika ombi hilo suala ambalo limesababisha kuitishwa kwa mkutano mkuu wa dharura.

23.2.2.  Mkutano Mkuu wa dharura utahudhuliwa na watendaji wote wa FENLZ, wanachama hai (waliolipa ada na kiingilio), wanachama waanzilishi, wanachama wa heshima na wageni waalikwa.

23.2.3.  Mkutano Mkuu wa dharura unaweza kuitishwa mara moja tu (1) kwa mwaka.

 

 

24.  UENDESHAJI WA VIKAO:

 

24.1.  Taarifa ya mkutano mkuu wa kawaida itatolewa kwa kila mwanachama si chini ya siku kumi na nne (14), na taarifa ya mkutano mkuu wa dharura itatolewa kwa wanachama si zaidi ya siku saba (7), kabla ya siku ya mkutano husika.

24.2.  Wanachama watakaotaka kuleta mawazo/ agenda maalumu kwenye Mkutano Mkuu, watatoa taarifa ya maandishi kwa katibu wa FENLZ siku saba kabla ya siku ya mkutano.

24.3.     Nusu ya idadi ya wanachama halali wa mkutano mkuu watakamilisha akidi (Quorum) ya mkutano wowote ule isipokuwa kwamba akidi haitahitajika endapo Mkutano umetokana na mkutano ulioahirishwa; endapo wanachama watakao kuwepo watachukuliwa kutosheleza akidi.

24.4.     Katika mkutano unaotokana na mkutano ulioahirishwa hautaruhusiwa kufanya maamuzi yoyote ya kubadili katiba ya FENLZ.

24.5.     Endapo saa moja na nusu itapita tangu muda uliokubaliwa kuwa ndio wa kuanza mkutano bila idadi ya wajumbe kutimia ili kuweza kufanya mkutano; basi mkutano uta ahirishwa na Mwenyekiti au makamu mwenyekiti hadi siku kama hiyo wiki inayofuata.

24.6.     Mwenyekiti ndiye atakayeongoza mikutano ya Kamati ya Utendaji, Mkutano Mkuu na Mkutano Mkuu wa dharura.

24.7.     Makamu mwenyekiti ataongoza shughuli za mikutano kama mwenyekiti hayupo.

24.8.     Endapo Mwenyekiti na makamu mwenyekiti hawakuhudhuria basi mjumbe mmoja anaweza kupendekezwa kuwa mwenyekiti kwa wakati huo.

24.9.     Katika mkutano mkuu maamuzi yatatokana na kupiga kura kwa kuinua mikono juu isipokuwa kama wanachama walioko katika mkutano wanaamua kwamba kura zipigwe kwa siri (secret ballot).

24.10. Uamuzi utaonekena kuwa umepitishwa kwa idadi ya wingi wa kura kuunga mkono hata kama tofauti ni ya kura moja (Majority decision) isipokuwa kama kura ni kwa ajili ya  kubadili katiba basi kura ni lazima ziwe siyo chini ya theluthi mbili (2/3) ya idadi ya wanachama waliohudhulia kukubali.

24.11. Hakutakuwepo na upigaji kura ya uwakilishi (no voting by proxy)

24.12. Katika upigaji kura endapo kura zitafungana Mwenyekiti atakuwa na kura ya Mwisho (Casting vote

24.13. Ni budi Mwenyekiti aheshimiwe wakati wa mkutano

24.14. Uamuzi wa mwenyekiti katika kudhibiti mwenendo wa mkutano ni wa mwisho labda kama atapingwa na theluthi ya wajumbe.

24.15. Mwenyekiti anamamlaka ya kuingilia usumbufu wowote unaojitokeza wakati wa Mkutano au kumtoa nje mjumbe ambaye anasumbua mwenendo wa mkutano.

24.16. Mjumbe atakayetolewa nje kwa ajili ya usumbufu atatakiwa aondoke eneo la Mkutano.

           

SEHEMU YA NANE.

  1.  SHERIA NDOGO ZA ASASI

25.1.     Mwanakikundi anatakiwa kuudhuria shughuli zote za kikundi.

25.2.     Simu ikiita kwenye kikao mwanachama atatozwa shilingi 500/=.

25.3.     Kudanganya faini ni shilingi 5000/=

25.4.     Kuchelewa kufika kwenye kikao faini ni shilingi 500/=

25.5.     Kupiga kelele au kuongea bila ruhusa ya kiongozi shilingi 1000/=

25.6.     Kutoudhuria kikao kimoja faini ni shilingi 500/=

25.7.     Mwanachama atakaye shindwa kulipa ada na michango katika kipindi cha mwaka mmoja atakuwa amejifukuza mwenyewe

25.8.     Kuwa mwaminifu, mwadilifu mkweli na kutetea msimamo wa FENLZ katika Maendeleo.

25.9.     Kuchangia mawazo kwa hali na mali katika kulinda Dira na Dhamira ya FENLZ.

25.10. Kukiuka maadili ya uanachama wa FENLZ kwa makusudi kutasababisha kusimamishwa au kuvuliwa uanachama wa FENLZ

25.11. Kwa kutenda kosa lolote ambalo wanachama wataridhia kwamba linafaa kumuondoa katika uanachama wa FENLZ na uamuzi huo kuridhiwa na mkutano mkuu.

25.12. Mwanachama atakaye fariki ndugu zake watapewa asilimia thelathini (30%) ya michango yake ya mwaka mmoja.

25.13. Mwanachama atakaye hama eneo atapewa asilimia thelasini (30%) ya michango yake ya mwaka mmoja

 

SEHEMU YA TISA

 MAPATO NA USIMAMIZI WAKE

 

26.  MAPATO, UHIFADHI NA UTOAJI WA FEDHA BENKI:

26.1.  Mapato ya FENLZ yanatokana na ada za uanachama, ada za kiingilio, michango ya wanachama, ruzuku na misaada ya wafadhili/ wahisani mbalimbali wa FENLZ.

26.2.  Mwaka wa fedha wa FENLZ utaanza tarehe 1 Januari na kuishia tarehe 31 Desemba ya kila mwaka

26.3.  Fedha zote za FENLZ zitawekwa katika tawi la benki litakalokuwa limeteuliwa isipokuwa fedha za matumizi madogomadogo zisizozidi 50,000/= zitahifadhiwa kwenye ofisi ya FENLZ (Kama Petty Cash).

26.4.  Waweka saini benki watakuwa wanne (4) ambao ni Mwenyekiti, Muhasibu na wajumbe wawili watakao chaguliwa na Bodi yaUshauri ambapo kati yao wawili watakuwa kundi “A”na wawili watakuwa kundi “B”.

26.5.  Fedha zitatolewa benki kwa kusainiwa na watu wawili mmoja kutoka kundi A na mmoja kutoka kundi B.

 

                                                                         SEHEMU YA KUMI:

 

MABADILIKO YA KATIBA, KUVUNJIKA NA LAKIRI YA ASASI.

 

27.  MABADILIKO YA KATIBA, KUVUNJA NA LAKIRI YA ASASI:

27.1.Mabadiliko ya Katiba:

Katiba haiwezi kubadilishwa au kufanyiwa marekebisho kwa namna yoyote ile isipokuwa kwa uamuzi utakao kuwa umefikiwa katika Mkutano Mkuu maalumu wa wanachama ambao utahudhuriwa na si chini ya theluthi mbili ya wanachama.

27.2.Kuvunjika kwa Asasi

27.2.1.  FENLZ itafikia ukomo kwa kuvunjika kama uamuzi huo utafikiwa na theluthi mbili ya wanachama waliohudhuria Mkutano Mkuu kupiga kura za kukubali uamuzi huo.

27.2.2.  Kama Mkutano utaazimia kuvunjika kwa FENLZ; utafanya utaratibu wa kulipa madeni yote ya FENLZ na hatimaye kumilikisha mali za FENLZ kwa asasi yenye makao yake mjini Katoro na yenye malengo yanayofanana na ya Asasi hii.

 

28.  MUHURI NA NEMBO YA FENLZ:

28.1.Kutakuwa na muhuri wa Asasi ambao ni wa duara na ndani yake utasomeka MARAFIKI WA ELIMU KANDA YA ZIWA na katikati ya maneno hayo kutakuwa na anuani ya FENLZ, S.L.P.           MWANZA.

28.2.Nembo ya FENLZ.

28.2.1.  Nembo ya utambulisho ya FENLZ itakuwa na watu wazima wawili wa jinsia zote walioshikana mikono kuwafunika watoto wawili wa jinsia zote na nyuma ya watoto kutakuwa na kitabu chenye kalamu katikati.

28.2.2.  Maana ya kuwa na alama hizi ni kwamba kwa kuwa na elimu; kutakufanya kuona mbali, kuwa na upeo mzuri wa matumizi ya anga, kutumia vyema rasilimali za nchi kavu na majini kwa manufaa ya Taifa.

28.2.3.  Kwenye nembo hiyo kutakuwa na maneno yanayosomeka Mtandao Wa Marafiki Wa Elimu Kanda ya Ziwa  *Friends Of Education Network Lake Zone (FENLZ).

 

SEHEMU YA KUMI NA MOJA

 

MENGINEYO:

29.  UWEZO WA KUJIUNGA NA TAASISI NYINGINE:

FENLZ inaweza kujiunga na Asasi ama Taasisi nyingine kwa kadri inavyofaa ili mradi uamuzi wa kujiunga na Taasisi au mitandao utaafikiwa na Bodi na wanachama watapata taarifa hizo kupitia kwenye Mkutano Mkuu.

 

30.  UTATUZI WA MIGOGORO:

Mgogoro wowote ndani ya FENLZ utakaoshindikana kupata usuluhishi ndani ya FENLZ, utaamuliwa na wanachama wa FENLZ katika Mkutano Mkuu na huo ndio utakuwa na madaraka na maamuzi ya mwisho.

 

UTHIBITISHO:

Sisi ambao majina yetu yameorodheshwa hapa chini na kutiwa saini zetu ndio wanachama waanzilishi wa Asasi ya Marafiki wa Elimu Kanda ya Ziwa (FENLZ) mwaka 2017. Kwa kutambua kuwa jamii inategemea juhudi za watu mbalimbali wenye ushirikiano ili kuleta maendeleo; tumeamua kwa ridhaa yetu kufanya uamuzi wa kuanzisha Asasi hii ambayo itafanya kazi kwa ushirikiano na jamii, wataalam mbalimbali na wadau kutoka serikalini na wadau wa nje ili kufikia malengo ya FENLZ na maendeleo ya Taifa.

 

Tutailinda, kuiheshimu, kuitetea na kuitunza Katiba hii ili itekeleze majukumu yake kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za kisheria za Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

 

No
JINA
SAINI
1
 
 
2
 
 
3
 
 
4
 
 
5
 
 
6
 
 
7
 
 
8
 
 
9
 
 
10
 
 

 

TUNATHIBITISHA KWAMBA HII NI NAKALA HALISI YA KATIBA YA FENLZ

**********************************************************************