Kurasa

Ijumaa, 30 Desemba 2016

MFAHAMU MRATIBU WA MTANDAO WA MARAFIKI WA ELIMU GEITA



MFAHAMU MRATIBU WA MTANDAO WA MARAFIKI WA ELIMU GEITA (MMEG/FENG) FRIEND’S OF EDUCATION NETWORK GEITA



KUZALIWA

AYUBU MZEE BWANAMADI ni kijana mwenye umri wa miaka 29. Amezaliwa katika wilaya ya Pangani mkoani Tanga nchini Tanzania Julia 1987.
ELIMU
Ameanza kusoma shule ya msingi Funguni wilayani Pangani mwaka 1996 na kuhitimu elimu yake ya msingi mwaka 2002. Na baada ya hapo kufanikiwa kujiunga na elimu ya sekondari katika shule ya sekondari FUNGUNI na kuhitimu kidato cha nne mnamo mwaka 2006. Baada ya hapo alijiunga na chuo cha mkoa cha ufundi stadi na huduma cha (RVTSC) VETA TANGA kwa upande wa fani ya uhazili na Tarakilishi (secretarial and Computer Course) kwa kipindi cha 2009 hadi 2010 kwa kuhitimu hatua ya tatu..
Baada ya hapo alijunga na chuo cha ualimu wa ufundi kilichopo  mkoa Morogoro Morogoro Vocational Teachers Training Collage (MVTTC) kwa kipindi cha masomo 2012/2013.

KAZI.
BWANAMADI alifanikiwa kufanya kazi kwa kujitolea katika halmashauri ya wilaya ya Pangani kama Katibu Muhtasi katika ofisi ya utumishi wilayani hapo kwa kipindi cha Desemba 2010 hadi april 2011. Pia alifanya kazi katika kampuni ya uuzaji na usambazaji bidhaa  ya Apex Market iliyokuwa jijini Tanga mtaa wa Majani Mapana mwaka 2007. Pia sehemu nyingine ya kazi ambapo amefanya kazi ni katika chuo cha ufundi stadi na huduma VETA Geita kuanzia mwaka 2014 Januari hadi 2016. 

HARAKATI ZA MARAFIKI WA ELIMU
Bwanamadi alijiunga na harakati za Marafiki wa Elimu mnamo mwaka 2005 akiwa kidato cha tatu katika shule ya sekondari Funguni iliyopo wilayani Pangani mkoani Tanga. Kwa zaidi ya miaka kumi kuanzia mwaka 2005 amekuwa akiendeleza Harakati za marafiki wa elimu. Kilichomvutia kujiunga na harakati hizi ni matangazo yaliyo kuwa yakirushwa na vyombo vya habari (video) ambayo mwisho yalikuwa yakileta hamasa kwa jamii kutaka kujua kipi kinacho endelea. Pamoja na vidokezo vya uelimishaji vilivyokuwa vikielimisha jamii kulikuwa na ujumbe usema “tuandikie rafiki@hakielimu.org”. Pamoja na anuani ya sanduku la barua kwa njia ya posta.

LENGO LA KUJIUNGA NA HARAKATI
Miongoni mwa malengo yaliyompelekea Bwanamadi kujiunga na harakati za Marafiki wa Elimu yalikuwa ni
1.    kuungana na wadau wengine wa elimu katika kuleta maendeleo chanya katika Nyanja hii ya elimu
2.    Kutoa elimu kwa jamii kadri ya muda na fursa inavyo patikana.
3.   Kusaidia jamii yenye uhitaji kadri ya muda na uweze atakao kuwanao.

MAFANIKIO
Katika uwepo wake ndani ya harakati hizi za marafiki wa elimu Bwanamadi amepata mafanikio mengi ikiwa ni kupata namba ya uanachama (membership number membership No: 318727) kutoka shirika la HakiElimu lenye makao makuu yake jijini Dar es salaam ambalo ni ndio Mraghabishi mkuu wa harakati za Marafiki wa Elimu Tanzania. Miongoni mwa mafanikio mengine ni:
a) Kuhamasisha wengine kujiunga na harakati hizi za marafiki wa elimu jambo ambalo ninaendelea kulifanya hadi sasa
b)   Kutoa elimu kupitia vyombo vya habari (redio na magazeti kama vile gazeti la Rai ambapo moja ya mada ilisema “kidole kimoja….” Mada ambayo ilikuwa ikihamasisha jamii kushiriki kikamilifu katika ujenzi wa shule za kata  na gazeti  la Mwananchi kwa mada isemayo “ Ikibidi mitaala ibadilishe baada ya miaka kumi” na redio ya Breeze FM na Mwambao FM zilizopo mkoani Tanga, Abood FM iliyopo mkoani Morogoro na Redio ya Storm FM iliyopo mkoani Geita.
c)    Kuanzisha maktaba ya jamii ambayo ilikuwa ikijulikana kwa jina la Mmadi Maktaba ambapo baadaye ilikuwa ikisimamiwa na kikundi cha marafiki wa elimu (Mwangaza Gombero) kilichopo kitongoji cha Gombero kata ya Pangani Mashariki wilayani Pangani mkoani Tanga.
d)   Kuwa ni mmoja wa waanzishi wa mitandao ya marafiki wa elimu nchini kwa kuanzisha mtandao wa kwanza wa marafiki wa elimu mkoani Tanga ambao ulikuwa ni mtandao wa marafiki wa elimu wilayani Pangani
e)    Kutembelea shuleni kufanya tafiti ya kubaini hali ya wanaochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza bila kujua kusoma kuandika na kuhesabu (kkk) na hii aliambatana na marafiki wa elimu kutoka kikundi cha marafiki wa elimu cha Mwangaza gombero huko wilayani Pangani. Pia kupima mpango wa matokeo makubwa sasa BRN na hii alikuwa mkoani Geita ambapo aliambatana na Marafiki wa Elimu Geita pamoja na wafanyakazi kutoka shirika la HakiElimu ambao ni Mr. Alinanuswe Kasyele, Mr. Raphaeli Kalonga na Mr. Pius Makomelelo ambapo ilikuwa ni mwaka 2015 na kushiriki na kuratibu zoezi la tafiti ya uwajibikaji na ushiriki wa wananchi katika maendeleo ya elimu katika maeneo ya Halmashauri ya Mji Geita mkoani Geita mwaka 2016.
f)     Kuwa kiongozi katika mitandao tofauti ya marafaki wa elimu kwa nafasi ya katibu wa mtandao wa marafiki wa elimu wilayani Pangani chini ya mwenyekiti Mzee Magendo (Kisport), Makamo Mwenyekiti wa mtandao wa mkoa wa marafiki wa elimu wa mkoa Tanga chini ya mwenyekiti mama Mariamu Makoko. Mshauri wa mtandao wa marafiki wa elimu wilayani na mkoani Morogoro chini ya mwenyekiti Islamu  Khasim Mposo. Katibu wa marafiki wa elimu Geita mji chini ya mwenyekiti ndugu Patrick Boniphace Mabula na hatimaye kuwa Mratibu wa mtandao wa marafiki wa elimu wilayani Geita chini ya mwenyekiti ndugu Alex Rwigi Kadaraja.
g)   Kuanzisha kilabu ya wapinga rushwa katika chuo cha ufundi stadi na huduma cha VETA TANGA.
h)   Kuwa Rais katika serikali ya wanachuo katika chuo hicho cha VETA TANGA.
i)     Kuwasaidia watoto yatima na wale wanaoishi kwenye mazingira magumu ambapo zoezi hili alifanya akiwa na kikundi cha Mwangaza Gombero chini ya mwenyekiti wake bi Amina Abdallah
j)     Kuhamasisha wanajamii walioanzisha vikundi ili kujiunga na harakati hizi na kupata marafiki wapya katika kijiji cha Katoro na Kamena wilayani Geita.
k)    Kupata nafasi ya kusimamia zoezi la utafiti juu ya uelewa kwa watoto lililokuwa likiendeshwa na asasi ya Uwezo na kuwa msimamizi msaidizi wilayani Pangani mwaka 2012
l)     Pia alitumia nafasi yake ya kazi na kufanikiwa kuanzasha klabu ya marafiki wa elimu katika chuo cha ufundi stadi cha Geita (Geita Vocational Training Centre) klabu ambayo imekuwa msaada mkubwa kwa mtandao wa marafiki wa elimu Geita ambapo kupitia klabu Mtandao wa Marafiki wa Elimu Geita (MMEG) uliweza kuandaa maeneo ya kufanyia vikao tofauti vya mtandao wa marafiki wa elimu Geita. Kuibua changamoto zinazo wakabili wanafunzi na kuzijadili kwa pamoja.
m)  Kushiriki katika kuandaa katiba ya mtandao wa marafiki wa elimu na kufanikisha usajili wa mtandao wa marafiki wa elimu Geita Friend’s of Education Network Geita (MMEG/FENG) kwa hatua ya asasi za kijamii (Community Based Organization –CBO) ngazi ya wilaya kwa kupatiwa cheti cha usajili na kusajiliwa kwa namba CBO.01335 katika halmashauri ya mji Geita.
             
CHANGAMOTO
“ni kweli kwamba kila jambo linachangamoto zake lakini kwangu changamoto katika harakati za marafiki wa elimu sizioni kuwa ni vikwazo vya kunizuia kufanya jambo nililolipanga bali huwa ni fursa ya ya kuniwezesha kutafaka njia mbadala ya kuweza kufika pale ninapo hitaji au kufanikisha lile ambalo nimelipanga.

MIKAKATI.
1.    Kujiimarisha vema katika harakati za marafiki wa elimu popote pale nitakapo kuwa katika utafutaji au matembezi ya kawaida kwa kujenga mahusiano ya karibu na wadau wa elimu na wanajamii kwa ujumla.
2.    Kuendeleza mtandao wa marafiki wa elimu Geita pamoja na mitandao mingine itakayo hitaji msaada wake kwa hali na mali ili kuisadia jamii katika maendeleo ya elimu.
3.    Kuendeleza harakati ndani ya mtandao wa marafiki wa elimu Geita na mitandao mingine hadi kufikia hatua ya asasi isiyo ya kiserikali (Non Government Organization NGO)
4.    Kujenga ushawishi kwa jamii na viongozi kujiunga na harakati za marafiki wa elimu na kuwa na mtazamo chanya katika maendeleo ya elimu katika maeneo yao.
 

OMBI
Ninawaomba marafiki wa elimu bila kujalisha  mtaa, kitongoji, kata, wilaya, mkoa ama tunatokea kanda gani tushirikiane vema katika kuleta maendeleo chanya juu ya elimu na demokrasia.
Pia ninaiomba jamii hususan walezi na wazazi kufuatilia vema maendeleo ya watoto wao (wanafunzi) wawapo maeneo ya shule ama nje ya shule zao kimaadili na kimazingira ili kuweza kuwasaidia wanafunzi na walimu kuinua taaluma za watoto (wanafunzi) hao.
Pia jamii ninaiomba kusoma machapisho yanayohusiana na masuala ya elimu ili kuweza kufahamu vema mahitaji na maendeleo ya elimu katika jamii zao
Pia ninaiomba serikali kuandaa falsafa ya elimu ya nchi yetu ya Tanzania kwa kipindi hiki tulichonacho ili kila mmoja aliyekuwa masomoni au nje ya masomo ajue kuwa anasoma kwa kutumia falsafa gani ya nje yake kama vile ilivyokuwa kwa wakati wa awamu ya kwanza “ujamaa na kujitegemea”
Mungu ibariki HakiElimu na wafanyakazi wake. Zibariki harakati za elimu na marafiki wake. Ibariki nchi yetu pendwa ya Tanzania.

MAWASILIANO         
Ayubu M. Bwanamadi
Mratibu wa Mtandao wa Marafiki wa Elimu Geita
S. L. P 45 Geita
Simu: +255765384115/+255714771883
               marafikiwaelimugeita@gmail.com

XXXXXXXXXX           DESEMBA 2016      XXXXXXXXXX

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni